Arusha,
Tanzania:
KITUO KIPYA CHA MPANGO WA �DREAM� Usa River ni eneo la kijijini, kaskazini mwa Tanzania, kilometa chache nje ya mji wa Arusha ambao umejikita katika masuala ya utalii na lenye mbuga kuu za wanyama
Katika njia inayoelekea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), kibao kidogo kinaashiria matumaini kwa eneo hili.
Kwa kukifuata kibao hiki utajikuta umeingia katika kichaka cha uoto wa asili, mahali ambapo mwezi mmoja tu uliopita kituo kipya cha DREAM cha kutibu UKIMWI
kilifunguliwa.
Kituo hiki kipya cha �afya� tayari kimekuwa kinatibu zaidi ya wagonjwa 140 nacho ni ishara ya matumaini kwa eneo hili.
Hapa VVU (Virusi vya UKIMWI) vinafikia 12%.
Baada ya Iringa, Arusha inakuwa kituo cha pili cha DREAM nchini Tanzania. Huku bado maeneo mapya yamechaguliwa kufungua vituo vingine. Hii ndiyo maana katika mwezi wa Agusti, katika mji wa Arusha, mafunzo kwa madakitari, manesi, wafanyakazi wa Afya, wakodinator na watumia computara watajifunza na kufuata muundo wa DREAM.
|